Psalms 75

Mungu Ni Mwamuzi

(Kwa Mwimbishaji: Kwa Ala Za Uimbaji Za Nyuzi. Zaburi Ya Asafu. Wimbo)


1 aEe Mungu, tunakushukuru,
tunakushukuru wewe,
kwa kuwa jina lako li karibu;
watu husimulia matendo yako ya ajabu.


2 bUnasema, “Ninachagua wakati maalum;
ni mimi nihukumuye kwa haki.

3 cWakati dunia na watu wake wote inapotetemeka,
ni mimi ninayezishikilia nguzo zake imara.

4 dKwa wale wenye majivuno ninasema,
‘Msijisifu tena,’
kwa wale waovu, ‘Msiinue pembe zenu.

5 eMsiinue pembe zenu dhidi ya mbingu;
msiseme kwa shingo zilizonyooshwa.’ ”


6 Hakuna yeyote atokaye mashariki wala magharibi
au kutoka jangwani awezaye kumkweza mwanadamu.

7 fBali Mungu ndiye ahukumuye:
Humshusha huyu na kumkweza mwingine.

8 gMkononi mwa Bwana kuna kikombe
kilichojaa mvinyo unaotoka povu
uliochanganywa na vikolezo;
huumimina, nao waovu wote wa dunia
hunywa mpaka tone la mwisho.


9 hBali mimi, nitatangaza hili milele;
nitaimba sifa kwa Mungu wa Yakobo.

10 iNitazikatilia mbali pembe za waovu wote,
bali pembe za wenye haki zitainuliwa juu.
Copyright information for SwhKC